FAHAMU JINSI YA KUFANYA BIASHARA KIPINDI CHA MAGUFULI



Sababu zinazowafanya watu kufunga frem kila kona ni nini?? 
"kabla ya yote ninamatatizo ya L& R. but niya yangu upate ujumbe".

Ninashindwa kuelewa kipindi hiki imekuwaje?? kuna nini?? kulikoni??  mbona kila pande za nchi ukipita maduka na frem nyingi zimefungwa?? eti watu wanadai maisha ni magumu. swali la kujiuliza je ukifunga frem ndo suruhisho sahihi la kuyafanya maisha yawe rahisi?? kama wewe ni mfugaji unahisi kuuza mifugo na kuchinja yote ni suruhisho sahihi?? na kama wewe ni mkulima unahisi kufungia jembe ndani ndio suruhisho la kufanya maisha kwako yasonge???

Hii inatokea kwa sababu watu wengi tulikuwa tumezoea kufungua biashara zetu kwa mazoea bila kujua mambo mhimu yanayotakiwa ktk biashara ni yapi?? Mtu anafuga lakin hajuwi anatumia njia gani ya kufuga au mtu analima hajui kesho mvua isiponyesha atafanyeje ili mazao yake yasiwe na shida.
wengi wetu tulikuwa tunafanya shughuri zetu za kibiashara kwa mazoea na bila tahadhari yoyote. bila ya kujua kwamba ktk biashara yoyote ile tahadhari ni kitu kikubwa sana. umewahi kujiuliza kwanini wataaramu wanatushauri tuwa na bima za biashara na afya zetu. hii ni kwa sababu ya tahadhari kwa chochote kitakacho tokea.
leo napenda kukujuza vitu vichache tu katika biashara:

naomba tuwe pamoja kwa haya. kwani katika biashara unatakiwa kujua mambo yafuatayo;
1.  Lengo la biashar: kwanini umeamua kufanya biashara hiyo?? kila mtu anayeanzisha biashara anatakiwa kuwa na lengo maalumu na biashara yake. kwani unapoanzisha biashara bila ya lengo maalum itakusumbua kujua unaelekea wapi katika biashara yako. wapo watu anafanya biashara ili mladi ck zisongee mbele. huyu mtu hana malengo yoyote na biashara hiyo just anafanya tu kwa mazoea. au kwa vile mama, shangazi au baba alikuwa anafanya kazi hiyo.[tubadilike].
2. Mipango ya biashara{business plan}: Lazima kabla ya hata kuanzisha biashara yako. upate mpango kazi wa biashara yako.{business pla}. hapa ndo uwanja wangu sasa wa kujidai. kwani watu wengi wamekuwa na tabia ya kufanya biashara bila mipango. namaanisha yakuwa kufanya biashara bila mipango ni sawa na kuuziwa mbuzi kwenye gunia. unfanya kitu ambacho hukijui au hukifahamu. hatari sana hii.
naomba twende pamoja: ndani ya business plan kuna vitu vya msingi unatakiwa kuvijua.kwa ufupi wake;[tubadirike].

(a) Masoko(market): kabla hata hujaanzisha biashara yako unatakiwa kujua soko lako ni lipi?? ndani ya kipengere cha masoko kuna vitu vya kuangalia  kama vile wateja wako ni kina nani?(your customers).  sehemu unapotaka kuanzishia biashara yako(location), matangazo(promotion/advisement ), bei (price) N.k viko vingin sana. kabla hujaanzisha biashara yako unatakiwa kuvijua vyote hivyo ili vikupe maamuzi yaliyo sahihi.[tubadirike].
(b). Usimamizi(management): watu wengi sana tumekuwa tukilia kuhusu biashara  zetu. kwani ni ukweli usiofichika yakuwa biashara ni usimamizi. sasa basi unapoanzisha biashara yoyote ili lazima ujue utawezaje kuisimamia?? ndipo utagundua kuna umhimu wa kuwa na management plan kabla ya biashara yako kuanza.hapa napo kuna mambo mengi sana ya kuangalia kwa leo siwezi kuyaelezea yote.[tubadirike].
(c). Uzalishaji(production): kama wewe biashara yako ni ya uzalishaji. kabla ya kufungua biashara yako unatakiwa kujua uzalishaji unaoenda kuufanya utakuwaje na kwa namna gani?? hata kama ni mandazi hiyo ni aina ya uzalishaji. lakini cha kushangaza tumekuwa tukifanya biashara zetu kwa mazoea.[tubadirike].
(d). kifedha(financial plan): lazima ujue mtaji ulionao na uweke mipango kulingana na mtaji wako. hapo utajua ni namna gani utaendesha mambo yako kwa mtaji ulionao. sio mtu unaanza biashara tu hujui hata garama za uendeshaji wa hiyo biashara yako.[tubadirike].

(e) Uendeshaji( operation): unatakiwa kujua garama za uendeshaji wa biashara yako kabla hata hujaanza biashara yako.yaani ukipiga picha kabla ya yote unatakiwa kuona kila kitu mbele kuna nini???. kwa mfano; kuna watu kisa tu anapesa za kununua mashine fulani baisi hajui hata huduma za mashine hiyo yaani maintenance. unakuta matu huyo ananunua mashine ambayo garama za kuihudumia ni zaidi ya kuinunulia. je huyo mtu kwa wakati kama huu atakuwa salama??? zaidi ya kufunga frem???[tubadirike].
3. Ubunifu (creativity): katika biashara lazima kuwe na ubunifu ili kuendana na mazingira na mabadiriko ya hali ya kiuchumi. usipokuwa mbunifu wewe katika maisha yako utakuwa msindikizaji tu na mtu wa kwanza kufunga frem. sio kwamba wote waliofunga frem hawana ubunif. no. ila ubunifu ni kitu mhimu sana katika biashara.[tubadirike].
Pamoja na sababu chache nilizoweza kuzielezea hapo juu!! nini tufanye ili kuendana na kasi ya MH.
1. Tubadirike kutoka kwenya hali ya mazoea na kuja kwenye hali ya uhalisia. usifanye kitu ili mladi tu unakifanya. inatakiwa kweli unadhamilia na kukiwekea mipango na malengo. kama ni biashara unatakiwa kuweka mipango madhubuti ya kutangaza biashara yako na uendeshaji[tubadirike].


2. Tufanye biashara kwa tija, tufuge kwa tija na tulime kwa tija: namaanisha tufuate taratibu za ufanyaji wa biashara na taratibu za ufugaji wa tija pia kulima kwa tija.[tubadirike].

3.wananchi tunatakiwa kuyafahamu haya na kuyajua kwa undani. kwani katika halimashauri zetu tunao wataaramu wetu. tuwatumie hao ili kutuelimisha yote haya. mabwana mifugo wapo, mabwana shamba wapo, maafisa biashara wapo. je kama wananchi hatuyafahamu haya wao wanafanya kazi gani huko maoffisi kwao???  kwani ni wajibu wao kutuelimisha sisi wananchi. au wao tunavyofunga frem zetu na kuchinja mifugo yetu wao wanafurahi?? tuwatumie hao ili tuweze kufuga kwa tija, kulima kwa tija na kufanya biashara kwa tija.[tubadirike].

mbali na hapo unaweza ukawasiliana na sisi kwa msadaa zaidi. ukatueleza unataka kufanya kilimo, ufugaji au biashara gani ili kukusaidia mawazo na mipango ni wapi pa kuanzia au wapi pa kuboresha kama una biashara yako tayari. tutakushauli kulingana na eneo ulipo na hali uliyonayo; kwani kwa uzoefu tumesaidia wengi.[tubadirike].
nawatakieni heri na baraka katika shughuri zenu za kila siku.
welcome to my blog. let us walk together.

Comments

1234 said…
Congratulations my brother you show the way all those who have influenced to try
Eng. NDAKI said…
Pamoja kiongozi. Kwani Niya yetu sote ni kuijenga nchi yetu.
Welcome to my blog. Let us walk together.
Unknown said…
Congrats and thanks alot bro,,,Allah akuzidishie na atuzishie maarifa na moyo wa kujiajir
Eng. NDAKI said…
Getting you Asha. Welcome to my blog. Let us walk together.
Kazini said…
Kaka Mungu akubariki ufike mbali kaka. You really bless me.
Eng. NDAKI said…
getting you mr. michael chacha. welcome to my blog. let us walk together.

Popular posts from this blog

CHALLENGE IS PART OF HUMAN LIFE